Social Icons

Pages

Blogger templates

Wednesday, February 3, 2016

Viwanda 366 vilivyokuwa vikifanya kazi 1984 vimekufa


Mbunge wa Momba David Silinde amesema kwamba viwanda 366 vilivyokuwa vikifanya kazi nchini mwaka 1984 vimekufa jambo linalosababisha vijana kukosa ajira nchini.

Mbunge ameyasema hayo wakati akitoa mchango wake wa mpango wa serikali wa mwaka 2016&2017 bungeni Dodoma

Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere alituachia viwanda 366 vikiwa vinafanya kazi kati ya hivyo viwanda vya kubangua korosho vilikuwa 12,viwanda vikubwa vya nguo 12 na vingine vingi lakini mpaka hivi sasa viwanda vya serikali vya kufanya kazi hizo hakuna vilibinafsishwa na vingine vimebakia magofu.

Silinde ameongeza kuwa kipindi hicho hicho shirika la ndege nchini lilikuwa na ndege zinazofanya kazi 11 sasa hivi ndege ipo moja na serikali jitihada zake kila mwaka hazionekani zikizaa matunda kunusuru hali hiyo.

Hata hivyo Mbunge huyo amesema serikali bajeti yake ni ndogo kuliko hata bajeti ya kuendesha taifa la Kenya na bado bajeti inategemea wahisani hivyo lazima serikali haitaweza kukamilisha miradi iliyojiwekea.

 

No comments:

Post a Comment