Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Wadau
wa mbolea wameaswa kuangalia namna ya kuboresha sheria na kanuni za
kusimamia sekta ya mbolea kwa manufaa ya wananchi wanaojishughulisha na
kilimo ili kiwe na tija kwa Watanzania na taifa kwa ujumla.
Kauli
hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
Dkt. Florence Turuka alipokuwa akifungua mkutano wa wadau wa mbolea
uliofanyika leo jiji Dar es Slaam.
Dkt.
Turuka amesema kuwa maeneo ya kuzingatiwa katika warsha hiyo ni pamoja
na kuboresha sheria na kanuni zinazosimamia sekta ya mbolea ili
kuwezesha sekta binafsi kushiriki katika kuinua kilimo kwa manufaa ya
Watanzania.
Gharama
hizo zinahusisha kufanyiwa majaribio mbolea zinazotoka nje ya nchi
kabla ya kuanza kutumiwa na wakulima ambapo majaribio hayo yanafanyika
kwa misimu mitatu ya kilimo.
Maeneo mengine ya kurekebisha ni pamoja na mlolongo wa tozo ambazo zimekuwa zikitozwa kwenye mbolea inayoingizwa nchini.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika linalojishughulisha na matumizi
ya mbolea Bara la Afrika anayesimamia eneo la Tanzania Dkt. Mshindo
Msolla amesema kuwa kazi kubwa waliyonayo wajumbe katika warsha hiyo ni
kuhakikisha sheria na kanuni wanazozifanyia kazi zitasaidia kuboresha
upatikanaji wa mbolea zenye ubora unaotakiwa kulingana na mahitaji ya
wakulima na waipate kwa wakati.
“Wakulima
hapa nchini wananufaika na huduma zetu ambazo tunatoa ikiwemo
kuwaunganisha na mawakala wakubwa wa pembejeo na makampuni yanayozalisha
au kuingiza mbolea nchini” alisema Dkt. Msolla.
Kuhusu
hali ya upatikanaji wa mbolea nchini, Dkt. Msolla amesema kuwa shirika
hilo linatoa huduma katika mikoa 12 nchini ambapo wapo mawakala 30
wanahudumia mawakala wadogo 500.
Mikoa hiyo ni Arusha,Kilimanjaro,Manyara, Morogoro, Iringa, Njombe, Mbeya, Ruvuma, Rukwa, Katavi na Kigoma.
Mawakala
hao msimu wa mwaka 2014/2015 wamefanikiwa kuuza kwa wakulima mbolea
tani 60,000 na mbegu tani 3000 ambazo zimekuwa na manufaa katika
kuhakikisha upatikanaji wa mazao ya chakula na biashara nchini.
Aidha,
shirika hilo limefanikiwa kuwaunganisha wakulima na makampuni ya mbolea
sita ikiwemo YARA, Extra Trading, Premium Agrochemical pamoja na
Minjingu.
Vile
vile, Dkt. Msolla amesema kuwa wakulima wamenufaika na kujengewa
maghala 14 hadi sasa yameanza kutumika ambayo yanauwezo wa kuhifadhi
tani 50,000 kwa wakati moja hatua ambayo inasaidia kusogeza huduma
karibu na wakulima wanapozihitaji.
Dkt.
Msolla amesema kuwa Shirika hilo lenye makao yake makuu Afrika Kusini
linatoa huduma kwa sekta ya mbolea katika nchi mbalimbali Barani Afrika
ikiwemo nchi tatu za kipaumbele ambazo ni Tanzania, Msumbiji na Ghana,
nchi nyingine ambazo shirika hilo linafanya kazi ni Ethiopia, Senegal,
Ivory Coast na Nigeria.
No comments:
Post a Comment