Na Benedict Liwenga
SERIKALI
imesema itaendelea kusogeza huduma za Zimamoto na Uokoaji kwa wananchi
kwa jinsi hali ya upatikanaji wa fedha itakavyoruhusu.
Kauli
hiyo imetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mhandisi Hamad Masauni wakati akijibu swali
la Mbunge wa Tunduma, Mhe. Frank Mwakajoka ambaye alitaka kujua ni lini
Serikali itapeleka huduma za Zimamoto katika Mpaka wa Tunduma ili
kuokoa mali za wafanyabiashara wanaosubiri kuvuka pindi ajali ya moto
inapotokea.
Mhe.
Msauni ameeleza kuwa, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika Halmashauri
ya Mji wa Tunduma lina Kituo katika eneo la mtaa wa Kilimanjaro, Wilaya
ya Momba katika Mkoa wa Songwe kinachohudumia Wilaya yote ukiwemo Mpaka
wa Tunduma.
"Kwa
sasa Kituo hiki kina gari moja lililopo matenegenzo Jijini Mbeya, hata
hivyo askari wanaendelea kutoa elimu ya Kinga na tahadhari ya Majanga ya
Moto na utumiaji wa vifaa vya huduma ya kwanza vya uzimaji moto",
alisema Masauni.
Aliongeza
kuwa, sambamba na ukaguzi wa majengo ya kutoa ushauri kwa kandarasi au
makampuni ya ujenzi kuhusu ujenzi bora wa miundombinu yenye usalama kwa
umma.
"Ni
azma ya Serikali kupeleka huduma ya Zimamoto katika maeneo yote ya nchi
ikiwemo Tunduma, hata hivyo azma hii nzuri inategemea na upatikanaji wa
rasilimali fedha, Serikali itaendelea kusogeza huduma za Zimamoto na
Uokoaji kwa wananchi kwa jinsi hali ya upatikanaji wa fedha
itakavyoruhusu", aliongeza Masauni.
No comments:
Post a Comment