Na Mwandishi Wetu, Songwe
Mbunge
wa Nzega Vijijini ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashahuri Kuu ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) Taifa, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla ambaye ni Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, ametembelea
kujionea maendeleo ya ujenzi wa Boma la jengo la ofisi za chama hicho
kwa Mkoa wa Songwe huku akichangia kiasi cha shilingi Laki Tano.
Dk.
Kigwangalla ambaye yupo kwenye ziara ya kikazi kwenye Mkoa huo mpya kwa
ajili ya kukagua huduma za Afya ambapo alipata wasaha huo wa kutembelea
jengo hilo na kueleza kuwa Serikali ya awamu ya tano ya CCM,
itaendelea kuboresha huduma bora za afya kama Ilani inavyosema ambapo
aliwataka wananchi kuendelea kumuunga mkono Rais Magufuli katika juhudi
zake mbalimbali za kulinda rasilimali za nchi.
“Rais
wetu ameongeza bajeti ya dawa kwa kiasi kikubwa huku mpango wa kuokoa
vifo vya akina Mama wajawazito na watoto wachanga tukilisimamia kwa
nguvu zote.. Hii ni sera yetu na tuendelee kukiunga mkono chama chetu”
alieleza Dk. Kigwangalla na kisha alichangia kiasi cha Tsh. 500,000,
kama mchango wake kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya ujenzi huo wa
jengo hilo la CCM Mkoa wa Songwe.
Mbali
na kutembelea ofisi hizo za CCM, Dk. Kigwangalla alipata wasaha
wakukagua Hospitali ya Vwawa na vituo mbalimbali vya Mkoa huo ikiwemo
kituo cha Afya Mbuyuni na Iyula.
Wakati
huo huo, Dk. Kigwangalla amemwagiza Mkurugenzi wa Wilaya ya Mbozi,
Eliasey Ngowi kukamilisha boma la chumba cha upasuaji linalojengwa
katika kituo cha Afya Iyula na ujenzi wake ukamilike ndani ya miezi
mine.
“Nakuagiza
Mkurugenzi boma ili la upasuaji likamilike ndani ya miezi mine. Na
nitakuja hapa kulizindua mimi mwenyewe, ukae kwenye vikao vyenu huko na
kushirikiana na Mbunge wa hapa, wananchi na hao wahisani muliowapata na
mukamilishe haraka sana” alieleza Dk. Kigwangalla.
Aidha,
alipongeza juhudi za watumishi wa sekta ya Afya kwa kuendelea kutoa
huduma bora huku akimwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe kuhakikisha
anakamilisha mifumo ya maji ndani ya chumba cha upasuaji, Maabara na
wodi ya Wazazi kwenye hospitali hiyo ya Vwawa.
No comments:
Post a Comment