UTAMADUNI WA KUFANYA KAZI NI NJIA YA KUFIKIA LENGO
LA TANZANIA YA VIWANDA.
Na Zawadi Msalla-WHUSM
Watumishi
wa Mkoa wa Songwe wameshauriwa kuwa na utamduni wa kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni nyenzo muhimu ya kufikia
malengo na azma iliyowekwa na Serikali ya awamu ya tano ya kuifanya Tanzania
kuwa nchi ya Viwanda.
Hayo
yamezungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel wakati alipokutana
na Sekretarieti ya Mkoa huo,na kuwaeleza kuwa ni wakati muafaka kwa watumishi kupata na kutoa elimu sahihi ya kuwafanya wananchi wapende
utamaduni wa kufanya kazi kwa bidii bila kulazimishwa.
”
Ni vizuri watumishi wakawa na elimu ya kutosha kuhusu utamaduni wa kufanya kazi
kwa bidii na kuzingatia maadili ya kiutumishi ili kuweza kuwaelimisha wananchi
umuhimu wa kufanya kazi kwa maendeleo ya nchi yetu” alisema Prof.Gabriel
Prof.
Elisante aliongeza kuwa ni muhimu kwa watumishi wa Umma na watanzania kwa ujumla
kufanya kazi kwa kushirikiana ili kutekeleza
majukumu yao ya kila siku kwa manufaa ya taifa .
Aidha
alieleza kuwa ni budi Watanzania kufuata maadili na kuzingatia muda katika utunzaji wa rasilimali za nchi kwa manufaa ya kizazi
kilichopo na kijacho kwa kuwa ni vigumu kutegemea mtu kutoka nje ya nchi kutunza rasilimali za nchi yetu.
Vilevile
Katibu Mkuu Prof.Elisante aliwaomba watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Songwe kuunga mkono jitihada za Rais John
Pombe Magufuli za kuipeleka mbele nchi katika uchumi wa kati na kuwa Tanzania
ya Viwanda.
Mbali na hayo Prof.Elisante aliipongeza Wilaya
ya Ileje kwa kuwa mfano katika utendaji uliopelekea mafanikio makubwa kwa mkoa wa Songwe na
kuzitaka Wilaya nyingine kuiga mfano huo.
Naye
Kaimu Katibu Tawala Mkoa Bw.Herman Tesha aliahidi kutekeleza ushauri ulitolewa
na Katibu Mkuu Prof.Elisante licha ya uchanga wa mkoa wake kwa kuwa anaamini mwamko na ari ya watumishi waliopo
kwa pamoja wanaweza kuleta maendeleo.
MWISHO
No comments:
Post a Comment