Wananchi
wa Kata ya Itaka Kijiji cha Itaka wengi wao wakiwa ni akina Mama,
wakijificha Mvua nje ya moja ya Kituo cha Usajili wakati wakishiriki
zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa linaloendelea kwenye Kata hiyo
Afisa
Usajili Mamlaka ya Vitambilsho vya Taifa akichukua alama za Vidole vya
mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Mbonji waliofika Katika moja ya Vituo
vya Usajili ili kupatiwa huduma ya usajili na Utambuzi.
Wananchi
wa Kijiji cha Mbonji kata ya Itaka Wilaya ya Mbozi wakiwa katika foleni
kuelekea kupata huduma ya Usajili na Utambuzi wa watu yenye lengo la
kuwapatia Vitambulisho vya Taifa, zoezi linaloendela katika kata nzima
ya Itaka.
Wananchi wa Kijiji cha Nsani wakiwa nje ya Kituo cha Usajili wakisubiri kupata huduma ya Usajili na Utambuzi.
Wananchi
wakiendelea na zoezi la kuchambua fomu nje ya Kituo cha Usajili katika
kijiji cha Nsani Kata ya Itaka Wilaya ya Mbozi kabla ya kwenda kupatiwa
huduma ya Usajili na Utambuzi uliohusisha uchukuaji wa alama za
kibaiologia, saini ya kielektroniki pamoja na Picha.
Wananchi
wa Kijiji cha Mbonji kata ya Itaka Wilaya ya Mbozi wakiwa katika foleni
kuelekea kupata huduma ya usajili na utambuzi zoezi linaloendela katika
kata nzima ya Itaka.
Pamoja
na zoezi la Usajili linalohusisha ujazwaji wa fomu za maombi pamoja na
kuchukuliwa alama za Kibaiologia pamoja na Picha, Mkoa wa Songwe umeanza
zoezi msingi la Mapingamizi ambapo wananchi wanapata fursa ya kuhakiki
taarifa zao pamoja na kuweka mapingamizi kwa mtu yoyote wanayehisi si
raia au si Mkazi wa eneo husika na amefanya udsajili wa maombi ya
Kitambulisho cha Taifa, ambapo Bi. Coletha amewasihi Wananchi wa
katanganyifu kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa.
Zoezi
hili lililoanza sambamba na kuendelea kwa usajili kwa Kata ambazo
hazijakamilisha linahusisha Kata za ichenjezya, vwawa na mlowo Wilayani
Mbozi mkoani Songwe baada ya kukamilisha hatua ya awali ya usajili.
Kwa
mujibu wa Afisa Usajili Wilaya ya Mbozi Bi. Bi. Coletha Peter amesema
zoezi hilo litahusisha wananchi wote wa mkoa wa Songwe na kuwataka
kujitokeza kwa wingi kwenye mbao za matangazo ambako picha zote za
waombaji wa Vitambulisho vya Taifa zimebandikwa pamoja na majina yao.
Amesema
kama Mamlaka wamejipanga kuhakikisha wanapokea mapingamizi ya watu wote
watakao bainishwa kwa njia ya wazi na siri na kuhakikisha Mamlaka
inayafanyia kazi majina hayo mapema sambamba na kuanza uchakataji wa
taarifa za waombaji wote waliokamilisha taratibu za Usajili ili
vitambulisho vianze kutolewa kwa wakati.
“
Tumepanga siku 7 za mapingamizi ambazo ni fursa pia kwa wananchi
kurekebisha taarifa zao iwapo watabaini kuna mapungufu yoyote na baada
ya hapo hatutatoa nafasi tena ya mtu kurekebisha taarifa. Mbali na
kurekebisha taarifa tunawaomba wananchi kuweka mapingamizi kwa wale wote
ambao watakuwa wamesajiliwa na hawana sifa za kupewa vitambulisho vya
Raia ili tuwaengue mapema kwenye mfumo” alisisitiza
Mkoa
wa Songwe ni miongoni mwa mikao 16 ya Tanzania Bara inayoendelea na
zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa na kwa Wilaya ya Mbozi mbali na
kuanza mapingamizi Kata za Isandula, Itumpi, Kilimampimbi, ipunga na
kata ya Itaka ndiyo zinaendelea na zoezi la Usajili kwa sasa.
Amesema
baada ya kukamilika Kata hizo awamu ijayo itahusisha Kata za Nambizo,
Magamba, Nanyala na Ruanda na kuwasititiza Wananchi ambao hawajafikiwa
na zoezi kuvuta subira na kuendeela kujiandaa kwa zoezi hilo ikiwa ni
pamoja na kuandaa Viambatanisho msingi vinavyotakiwa katika zoezi la
Usajili na Utambuzi wa Watu.
Mikoa
mingine inayoendelea na zoezi la Usajili ni Mara, Mwanza, Arusha,
Kilimanjaro, Manyara, Singida, Geita, Shinyanga, Simiyu, Mtwara, Lindi,
Ruvuma, Njombe, Iringa na Mbeya.
No comments:
Post a Comment