Social Icons

Pages

Blogger templates

Thursday, February 22, 2018

"NI BORA TUKAWIE LAKINI TUFIKE" MHE BITEKO


Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua kinu cha kuchakata dhahabu mara baada ya kutembelea mgodi wa uchimbaji dhahabu wa Shanta Gold Mine uliopo katika Kijiji na Kata ya Saza akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Songwe, Leo 22 Februari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal-Wazo Huru Blog
Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua baadhi ya mitambo ya uchenjuaji madini katika mgodi wa uchimbaji dhahabu wa Shanta Gold Mine uliopo katika Kijiji na Kata ya Saza akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Songwe, Leo 22 Februari 2018.
Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua njia ya kwenda kwenye mgodi wa chini mara baada ya kutembelea mgodi wa uchimbaji dhahabu wa Shanta Gold Mine uliopo katika Kijiji na Kata ya Saza akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Songwe, Leo 22 Februari 2018.
Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akizungumza na wafanyakazi wa mgodi wa Shanta uliopo katika Kijiji na Kata ya Saza Wilayani SongweLeo 22 Februari 2018.

Na Mathias Canal, Songwe

Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko amesifu utendaji unaofanywa na kampuni ya uchimbaji madini ya dhababu wa Shanta Gold Mine kwa kukubali kuendana na matakwa ya serikali kwa kufuata kanuni, taratibu na sheria za nchi katika sekta hiyo.

Alisema kuwa Wizara hiyo imedhamiria kuboresha sekta ya Madini ili wananchi waweze kunufaika na rasilimali hiyo ambayo imechezewa na wajanja wachache katika kipindi cha muda mrefu.

Mhe Naibu Waziri huyo ametoa kauli hiyo Leo 22 Februari 2018 wakati akizungumza na wafanyakazi wa mgodi wa Shanta uliopo katika Kijiji na Kata ya Saza Wilayani Songwe.

Kampuni ya SGM haipo kwenye kundi la wawekezaji walalamikaji kuwa serikali kupitia sheria ya madini inawakimbiza wawekezaji jambo ambapo sio kweli badala yake serikali imeweka utaratibu yakinifu wa uchumi fungamanishi utakaoboresha sekta ya Madini na kuwanufaisha watanzania.

"Twendeni kwa watanzania tukawaulize wamenufaika  kwa kiasi gani na uwepo wa migodi mbalimbali ya uchimbaji nchini, jibu ni jepesi tu kuna watu wachache wamenufaika na rasilimali hiyo jambo ambapo hatutalifumbia macho tena" Alisema Mhe Biteko na kuongeza kuwa

"Serikali inahitaji wawekezaji ambao wanafuata sheria Na taratibu za nchi hata kama ni wachache wanapaswa kufahamu kuwa wanapaswa kufuata sheria kwani kufanya hivyo sio ombi bali ni lazima"

Aliongeza kuwa Wizara ya Madini itaendeleza ushirikiano kwa kiasi kikubwa na mgodi huo ili kuinua zaidi uwekezaji wao na hatimaye kuwa na uzalishaji wenye tija ambao utapelekea serikali kukusanya kodi kwa kiasi kikubwa kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla wake. 

Alisema kuwa watumishi wote katika Wizara ya Madini na wawekezaji katika sekta ya madini wanapaswa kusimamia haki katika utendaji wao huku wakiunga mkono juhudi za serikali katika kuimarisha nidhamu ya uwajibikaji hususani kujitenga na utoaji ama upokeaji wa rushwa.

Alisema dhamira ya serikali ya awamu ya tano ni kuwarahisishia huduma wachimbaji wadogo kupitia malezi bora ya Wizara ya madini ili kufikia hatua ya kuwa wachimbaji wa kati na hatimaye kufikia uwekezaji mkubwa katika uchimbaji wa rasilimali hiyo.

Katika hatua nyingine wawekezaji hao wametakiwa kuwaamini wataalamu wa Madini wa hapa nchini pasina kuwa na Mashaka nao kwani serikali inawafahamu na wengi wao wakiwa wanafanya kazi nje ya nchi.

No comments:

Post a Comment