Mbunge Viti Maalum, Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza, akizungumza na Wajumbe wa Jumuiya ya wanawake wa CCM, (UWT) wilaya ya Mbozi, jana mchana mjini Vwawa, wilayani Mbozi, Shonza alikutana na wajumbe hao kwa lengo la kutoa shukrani zake kumuamini na kumpatia ubunge katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka jana.
Mbunge Viti Maalum, Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza,(mwenye nguo nyekundu) akicheza na Wajumbe wa Jumuiya ya wanawake wa CCM, (UWT) wilaya ya Mbozi, jana mchana mjini Vwawa, wilayani Mbozi, Shonza alikutana na wajumbe hao kwa lengo la kutoa shukrani zake kumuamini na kumpatia ubunge katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka jana
Mbunge
wa Viti Maalumu, Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza amewataka wanawake wa
Wilaya ya Mbozi na mkoa kwa ujumla kumtumia ipasavyo kuwasilisha kero
zao ili akawapiganie bungeni kwani ndio kazi alioomba.
Shonza
alitoa rai hiyo jana wakati akitoa shukrani zake kwa wajumbe wa
Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT) Wilaya ya Mbozi, mkoani hapa kumuamini
na kumpatia kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana kupitia chama hicho.
Alisema
kama walivyomuamini kwa kumpatia kura nyingi zilizomuwezesha kupata
ubunge, ndivyo wanavyotakiwa kumtumia katika kipindi chote cha uongozi
wake huku akiomba ushirikiano wa dhati kutoka kwao (wananchi) kwenye
utekelezaji wa majukumu ya kijamii ikiwamo miradi mbalimbali
anayotarajia kuifanya.
Shonza
alisema anafahamu changamoto zinazowakabili wananchi wa Mbozi,ikiwamo
umeme hususani vijijini, pembejeo za kilimo, maji na mawasiliano hivyo
wampe ushirikiano na anakwenda bungeni kupigania mambo hao muhimu kwani
mawaziri wengi ‘anawamudu’.
Aliwataka
wananchi hao kujiunga kwenye vikundi iwe rahisi kusaidiwa kwa kupatiwa
mikopo na misaada mingine ambayo itawasidia kukuza vipato vyao, kwani
huu ni muda wa kuwezeshana hususani wanawake ambao ndio nguvu kuu ya
familia.
Alisema
‘Hivi sasa huwezi kupata mkopo mtu binafsi ni lazima ujiunge kwenye
kikundi, hivyo basi leo kwa kuanzia natoa Sh600,000 kwa ajili ya
kusajili vikundi vyenu, kwa vile ambavyo vipo tayari lakini
hamjavisajili. Ila huu ni mwanzo tutafanya mambo mengi na mazuri
zaidi’.
Mwenyekiti
wa UWT, Wilaya ya Mbozi, Issabela Mbaya alisema umoja huo utamtumia
Shonza kuleta umoja na maendeleo kwa wanawake wa wilaya hiyo.
KWA HISANI YA MICHUZI MEDIA
KWA HISANI YA MICHUZI MEDIA
No comments:
Post a Comment